Informações:
Sinopsis
Makala ya kila siku yanayompa fursa msikilizaji kutoa maoni yake juu ya habari zilizopewa uzito wa juu kwa siku husika. Msikilizaji hushiriki kwa kutuma ujumbe mfupi pamoja na kupiga simu.
Episodios
-
Haiti : Je polisi wa Kenya watafulu kuzima vurugu kule Haiti
26/06/2024 Duración: 09minKenya imetuma polisi wake nchini Haiti kwenda kujaribu kudhibiti magenge ya wahalifu ambayo yametatiza usalama wa taifa hilo kwa kipindi kirefu. Polisi wa Kenya wanaenda Haiti licha ya mataifa kama Marekani kushindwa kurejesha amani nchini Haiti.Je Polisi wa Kenya watafaulu? ndilo swali tumekuuliza.Haya hapa baadhi ya maoni yako.
-
Burundi : Uhaba wa mafuta wazidi kutatiza shughuli za usafiri
25/06/2024 Duración: 09minKatika makala haya tunaangazia taifa la Burundi linalozidi kushuhudia uhaba mkubwa wa mafuta, hili likitatatiza shughuli za usafiri katika taifa hilo la Africa mashariki. Tumekuuliza unafikiri nini huwa chanzo cha ukosefu wa mafuta katika mataifa yetu? Haya hapa baadhi ya maoni yako.
-
Nini kifanyike kutatua wimbi la wakimbizi Africa
24/06/2024 Duración: 10minKatika makala haya tunajadili maadimisho siku ya kimataifa ya wakimbizi, yaliofanyika juma lililopita ripoti zikionesha watu zaidi ya millioni 120 duniani wanakimbia mataifa yao kutokona na mizozo, uchumi mbaya na mabadiliko ya tabia nchi. Tumekuuliza nini kifanyike kukabiliana na wimbi la wakimbizi duniani? Haya hapa baadhi ya maoni yako
-
-
Matukio ya ajali za moto katika nchi tofauti Afrika Mashariki ikiwemo Bukavu DRC
14/06/2024 Duración: 10min -
Mvutano kati ya serikali ya Kenya kuhusu mafao ya rais mstaafu Uhuru Kenyatta
12/06/2024 Duración: 10minOfisi ya rais mstaafu Uhuru Kenyatta imelalamikia kuhujumiwa kwa kutopewa ufadhili unaofaa
-
Visa vya raia kuwashambulia maofisa wa polisi vimeendelea kuongezeka Afrika
12/06/2024 Duración: 10minKisa cha hivi punde nchini Kenya ambapo raia alimshambulia ofisa wa polisi ,kimeibua mjadala
-
Jukumu la jumuiya ya kimataifa kumaliza mzozo wa nchi ya Sudan
11/06/2024 Duración: 09minMashirika ya kutetea haki za binadaam yametuhumu jumuiya ya kimataifa kwa kushindwa kumaliza mzozo wa Sudan
-
-
Nini suluhu ya hali ya msongamano kwenye magereza ya nchi za Afrika Mashariki
06/06/2024 Duración: 09minNchini DRC, mashirika ya kutetea haki za binadamu yakitaka serikali kuboresha mazingira ili kuepuka vifo na ukiukwaji wa haki za wafungwa,mwaka uliopita, vifo zaidi ya 500 vilirekodiwa katika gereza kuu la makala nchini DRC.
-
Matarajio yako kuhusu mkutano wa kibiashara kati ya Korea Kusini na Afrika
04/06/2024 Duración: 09min -
Uchaguzi nchini Afrika Kusini, chama tawla ANC kupoteza wingi wa viti bungeni
04/06/2024 Duración: 09min -
Kila Ijumaa ni fasi yako mskilizaji kuchangia mada ndani ya rfi Kiswahili
18/05/2024 Duración: 10minKila siku ya Ijumaa rfi Kiswahili inakupa mskilizaji nafasi ya changai mada yoyote ambayo unapenda, liwe jambo linalofanyika hapo ulipo au yale umeskia katika taarifa wetu. Juma hili pamekuwa na matokeo mengi tu, katika ulingo wa siasan michezo, biashara, usalama na hata mazingira.Hii hapa baadhi ya michango yenu.
-
Je mataifa tajiri yanaweza saidia mataifa maskini kupata nishati safi
16/05/2024 Duración: 09minWiki hii Paris, ilikuwa mwenyeji wa mkutano wa Kimataifa kujadili namna ya kuyasaidia mataifa masikini hasa barani Afrika, kufikia malengo ya kukumbatia nishati safi ya kupikia na kuachana na mkaa na kuni. Ufaransa, imeahidi kutoa Euro Milioni 100 kusaidia kufikia malengo hayo ndani ya miaka mitano ijayo.Unaamini mataifa tajiri yatasaidia Afrika katika hili ?Serikali ya nchi yako inafanya nini kukumbatia matumizi ya nishati safi kama gesi ?Haya hapa baadhi ya maoni yako.
-
Somalia : Yataka ujumbe wa umoja wa mataifa wa kisiasa kuondoka
15/05/2024 Duración: 09minSerikali ya Somalia imeandikia bazara la usalama la umoja wa mataifa ikitaka ujumbe wa umoja huo ambao umekuwa ukisaidia serikali katika maswala ya kisiasa na usalma kuondoka. Hakuna sababu maalumu zilizotolewa na serikali ya Somalia, hapa tunakuuliza je ni sahihi kwa ujumbe huu wa umoja wa mataifa kuondoka kipindi hiki nchi hiyo ikizidi kupitia changamoto za kiusalama? Haya hapa baadhi ya maoni yako.
-
Ujuzi au vyeti, serikali ya Kenya inawasaka wafanyakazi waliotumia vyeti ghushi kupata ajira
14/05/2024 Duración: 09minSerikali ya Kenya inaendesha uchuguzi kuhusiana na madai ya baadhi ya wafanyakazi wake kumiliki vyeti ghushi, walivyotumia kupata ajira. Unafaikiri mtu anapaswa kuajiriwa kutokana na vyeti vyake au ujuzi wa kazi ?Nchini mwako ajira hutolewa vipi ?Haya hapa baadhi ya maoni yako.
-
Nini mchango wa masharika ya kirai katika mataifa yetu ya Africa
13/05/2024 Duración: 10minKongamano la kwanza la mashirika ya kiraia la Umoja wa Mataifa limekamilika jijini Nairobi wiki iliyopita, huku wito wa mazungumzo ya uwazi na ukweli kati ya serikali na mashirika hayo ukisisitizwa. Upi mchango wa mashirika ya kiraia kwenye nchi zetu?Unadhani yamefanya vya kutosha kuzisaidia jamii na kuchochea maendeleo?Kipi zaidi kifanyike kuboresha uhusiano kati yake na Serikali? Ski makala
-
Maoni ya waskilizaji kuhusu mafuriko yanayo zikumba nchi za Afrika mashariki
07/05/2024 Duración: 10minMafuriko yanashuhudiwa kwenye nchi za Afrika Mashariki, mamia ya watu wakiripotiwa kufariki, nyumba na miundombinu ikiharibiwa.Nchi za Kenya na Tanzania zimeathirika pakubwa na mafuriko haya. Unazungumziaje miakakati inayochukuliwa kuzuia madhara zaidi?Hali ikoje nchini mwako?Unachukua tahadhari zipi binafsi kujilinda?
-
-